Maazimio ya mkutano mkuu TAMSYA 2016/17



 MAAZIMIO YA MKUTANO MKUU (TAMSYA) 2016/17

BAADA YA KUPOKEA RIPOTI, TAARIFA NA MIJADALA MBALIMBALI KUTOKA MIKOA NA MATAWI YA JUMUIYA, MKUTANO MKUU UNAAZIMIA YAFUATAYO:
1. Tumeazimia kugawa mikoa kikanda na kupanga waratibu kutoka kamati kuu tendaji ya Taifa watakaoshirikiana na viongozi wa mikoa kusimamia miradi, kudhibiti upotevu wa mali za TAMSYA na kutatua migogoro katika mikoa husika.
2. Kuanzisha na kuboresha madrasa, kambi, program za tuisheni na somo la maarifa ya uislamu kwa shule za msingi na sekondari.
3. Kuimarisha mfumo wa upashanaji wa habari, kwa kutoa taarifa sahihi kwa wakati ili kuboresha mahusiano mema kwa wanajumuiya na jamii.
4. kusimamia na kutoa elimu sahihi juu ya vazi la hijabu, kutoa miongozo na nyaraka stahiki kuhusu vazi hilo.
5. Kusimamia na kuhuisha programu za dawah mashuleni,vyuoni kwa kushirikiana na taasisi rafiki.  



 VIPAUMBELE VYA MWAKA 2017.
i.                   Kusajili wanajumuiya na vikundi ndani ya jumuiya.
ii.                Kuboresha mahusiano ya kimkakati na jumuiya, asasi za kiraia na serikali.
iii.             Kujihusisha kwa kina katika mipango ya kuhuisha jumuiya ambayo ni:
ü Kufanya kambi maalumu za wanajumuiya.
ü Kufanya kambi za viongozi.
ü Semina na warsha kwa viongozi kuwajengea uwezo.
ü Kujihusisha na utoaji wa ushauri na nasaha kwa wanajumuiya.
iv.              Kufanya ziara za ndani na nje ya ofisi.
ü Ziara za matawini.
ü Ziara katika ofisi mbalimbali.
ü Kutembeleana katika program za makaribisho na kuwaaga wanajumuiya.
v.                 Kuboresha mahusiano mema na jamii.
ü Kutembelea na kutoa huduma kwa wagonjwa.
ü Vituo vya kulelela watoto yatima.
ü Magereza na kutembelea wafungwa.
ü Kutoa hotuba na da’awa misikitini na vituo vya kiislamu.
ü Kujitolea kutoa damu salama kwa wagonjwa.
ü Kutembelea vituo vya wazee.
ü Kupanda miti pamoja na kufanya usafi maeneo mbalimbali ya kijamii.
vi)Kuboresha na kusimamia utekelezaji wa majukumu ya idara ya wanawake.
Share on Google Plus

About UPStream Telecom

0 comments:

Post a Comment