LIJUWE LENGO NA MAANA YA KUSIMAMISHA SWALA


Maana ya Kusimamisha Swala.
Ni kuswali kwa kutekeleza kikamilifu nguzo, sharti zote za swala na kuwa na unyenyekevu (khushui) ndani ya swala.

Nafasi na Umuhimu wa Kusimamisha Swala katika Uislamu.
Swala imesisitizwa na ina umuhimu katika Uislamu kwa sababu zifuatazo;

i.             Kusimamisha Swala ni Amri ya Mwenyezi Mungu (s.w).
Mwenyezi Mungu (s.w) ameamrisha waumini (waislamu) wote wasimamishe swala zote za faradh na sunnah ipasavyo.
           Rejea Qur’an (29:45), (4:103) na (14:31).

  ii.            Kusimamisha swala ni nguzo ya Pili ya Uislamu.
          Baada ya shahada mbili, nguzo ya pili na ya msingi mno katika Uislamu ni kusimamisha swala.

iii.            Swala humtakasa muislamu na mambo machafu na maovu.
           Bila shaka swala ikiswaliwa vilivyo humuepusha mja na mambo machafu na maovu.
           Rejea Qur’an (29:45).

 iv.            Swala ni amali ya mwanzo kabisa kuhesabiwa siku ya Qiyama.
           Swala ya muumini ikitengemaa vizuri ndio sababu ya kufaulu kwake Duniani na Akhera pia.
           Rejea Qur’an (23:1-2,9), (87:14-15) na (22:34-35).

 v.           Kutosimamisha swala ni sababu ya mtu kuingizwa motoni.
         Hii ni baada ya muislamu Kupuuza swala kwa kutozingatia sharti na nguzo zake kikamilifu na kukosa unyenyekevu (khushui) ndani ya swala.
Rejea Qur’an (74:42-47), (68:42-43) na (107:4-5).


Lengo la Kusimamisha Swala.
Lengo kuu la kusimamisha swala ni kumkinga mja na mambo machafu na maovu kwa kutekeleza kikamilifu sharti, nguzo na sunnah za swala pamoja na kuwa na khushui ndani ya swala kama ifuatavyo;
i.                   Swala inamtakasa mja kwa kuzingatia na kutekeleza sharti zake zote kikamilifu ambazo ni kuwa twahara, sitara (kujisitiri), kuchunga wakati wa swala na kuelekea Qibla.

ii.                 Swala inamtakasa mja kwa kutekeleza kikamilifu nguzo na sunnah za swala kama kumsifu na kumtukuza Mwenyezi Mungu (s.w), kusoma Qur’an, kutoa ahadi ya kujisalimisha kwa Mwenyezi Mungu (s.w), kuomba dua na kutekeleza vitendo vyote vya swala.

Share on Google Plus

About Rajabu Athuman

0 comments:

Post a Comment